Wednesday, December 7, 2011

Santos wa Arsenal nje mechi ya Everton

Mlinzi wa kushoto wa Arsenal Andre Santos, ameondolewa katika kikosi kitakachocheza siku ya Jumamosi dhidi ya Everton katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu ya Kandanda ya England baada ya kuumia kifundo cha mguu wakati wa mchezo na Olympiakos.

Andre Santos aumia kifundo cha mguu hatacheza na Everton
Andre Santos
Santos alilazimika kutoka uwanjani dakika ya 51 siku ya Jumanne baada ya Arsenal kulazwa mabao 3-1 katika mchezo wa mwisho wa kundi lao la F kuwania kufuzu kwa hatua ya mtoano ya Ubingwa wa Ulaya.

Hhc Alive ina habari kuwa Santos, ambaye ameshacheza tangu mwanzo mechi 12 za Arsenal katika mashindano yote msimu huu, huenda akakosa mechi hiyo moja tu dhdi ya Everton.

Walinzi wengine wa pembeni wa Arsenal Carl Jenkinson, Kieran Gibbs na Bacary Sagna nao wagonjwa.

Gibbs anaendelea kupata nafuu baada ya kufanyiwa upasuaji wa mshipa wa ngiri mwezi uliopita na hatazamiwi kucheza mechi na Everton, wakati Jenkinson anakabiliwa na maumivu ya mgongo.

Sagna alivunjika mguu wakati Arsenal ilipolazwa na Tottenham mwezi wa Oktoba.

Wenger huenda akalazimika kumchezesha nafasi ya ulinzi wa kushoto Thomas Vermaelen kutokana na walinzi wa kutumainiwa wa pembeni karibu wote kuumia.

Santos, ambaye amshacheza mechi 22 za kimataifa kwa timu yake ya taifa ya Brazil, alijiunga na the Gunners msimu huu akitokea klabu ya Uturuki ya Fenerbahce kwa kitita cha paundi milioni 6.

No comments:

Post a Comment