Wednesday, December 7, 2011

Blessed are those who hunger and thirst

An amazing thing happens when we seek God's face! He ends up 'clothing' us with His righteousness and as the scripture in Matthew 6:23 says, adds all things unto us. As I was meditating on the word righteousness, the Spirit led me to search the word in my iPod NIV Bible. Some incredible threads leapt out at me and I decided to dig a little deeper.

I found something interesting in the following verses from John 16:7-11:
7: "But I tell you the truth: It is for your own good that I am going away. Unless I go away, the Counselor will not come to you; but if I go, I will send Him to you"
8:" When he comes, he will convict the world of guilt in regard to sin and righteousness and judgement."
9: "In regard to sin because men do not believe in me;
10: "In regard to RIGHTEOUSNESS (emphasis mine), because I am going to the Father, where you can see me no longer and in regard to judgement because the prince of this world now stands condemned."
John Kagaruki
When we look at the three items Jesus mentions, we see the Holy Spirit doing three things and there is righteousness in the middle of them, being positioned in such a manner as to suggest that the Spirit of God comes to dwell in us and thus clothe us with righteousness! 'In regard to righteousness, because' He is going to the Father where they can see Him no longer! The light bulbs go on! 'Seek ye first...' In Psalm 13:1 David asks how long the Lord will hide his face from him.

Paul in quoting the Psalms in Romans 3:10,11 says that 'There is no one righteous, not even one, there is no one who understands, no one who SEEKS God.'
So we find from John 16 that:
1. The sin that the Spirit convicts of is that of not believing in Him (It is by grace we are saved through faith...). Ephesians 2:8 & John 3:16, Galatians 5:5.

2. The righteousness that He convicts of is that of being with and in Him
(It seems strange that Jesus would deliberately equate righteousnesss with His not being seen any longer! When Jesus was with them, they walked with 'God'. He who has seen the Son, has seen the Father! 

3. The judgement He dishes out is to the prince of this world.
It then seems that we are truly blessed when we are filled with the Holy Spirit (God's manifest Presence in us) as this is what produces our righteousness by faith. Galatians 5:5 talks about us eagerly awaiting the righteousness for which we hope for by faith. 
From this arise the fruit of the spirit, the gifts of the spirit and the authority of the spirit! Malachi 4: 2,3: But for you who revere my name, the sun of righteousness will rise with healing in its wings. And you will go out and leap like calves released from the stall. 
(3) then you will TRAMPLE (emphasis mine) down the wicked! Connect this with Luke 10:19 where Jesus says 'I have given you authority to trample on snakes and scorpions and to overcome ALL (emphasis mine) the power of the enemy; nothing will harm you' ( Mark 16:17: And these signs will accompany....). Oh that we would seek His face and hide under his wings! (Psalm 91).
Do you want to get healed? Do you want to trample down demons and powers of darkness? This is not the monopoly of titled ministers of the Gospel! Does 'In the last days I will pour out my Spirit on ALL people...'(Joel 2:28) ring a bell? Then seek His face, hunger and thirst for His righteousness (The Counselor) and you will be filled!
By John Kagaruki.

Siri ya Marehemu Dr Remmy Ongala Kufuga Nywele



Dr Remmy Ongala akijisomea Neno la Mungu
Ramadhani Mtolo ndio jina halisi la Marehemu Dr Remmy Ongala, alikuwa Mwanamuziki wa nyimbo za Kidunia(Circular Music) na baadaye  alipata Neema ya Kumpokea Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wa Maisha Yake Miaka Michache kabla ya Kifo chake.

Dr Remmy Ongala alizaliwa nchini Congo Kinshasa mwaka 1947 katika mkoa wa Kivu, Mama yake mzazi alikuwa ameshajaliwa kujifungua watoto wawili ambapo kwa bahati mbaya wote walifariki. 

Watoto hawa hawakuwa Mapacha na aliwazaa katika vipindi viwili tofauti na kila mmoja alifariki kwa wakati tofauti. Mama huyo alipopata ujauzito wa tatu akaona inawezekana kabisa mtoto huyo akafariki kama walivyofariki wengine wawili waliotangulia.

Baada ya kujiuliza Maswali kwa muda mrefu pasipo majibu ndipo siku ya siku alijifungua mtoto wa kiume aliyempa jina la Ramadhani ambaye ndiye Remmy.Kwa kuwa mamaye  Remmy hakutaka kumpoteza  mwanaye, akaamua kwenda kwa mganga wa Kienyeji ili kupata Kinga itakayoyasalimisha maisha ya Mwanae.

Alipofika kwa Mganga wa Kienyeji, mganga alimwambia ili mtoto wake asifariki inabidi mtoto huyo(Remmy) asinyolewe nywele  Maishani mwake ushauri ambao mamaye aliupokea na kuufanyia kazi. Remmy alizaliwa akiwa tayari na meno mawili ya mbele kitu ambacho kilichukuliwa kama ishara ya baadaye kuja kuwa mganga wa kienyeji ingawa utabiri huo haukutimia. Hivyo toka akiwa mtoto mdogo Dr Remmy hakukatwa Nywele na hata alipokuwa mkubwa na kulijua hilo halikumsumbua sana kwa kuwa alikuwa keshazoea kuishi kwa staili hiyo.

Remmy aliingia nchini mwaka 1978 na katika kipindi chote hicho alikuwa akifanya kazi kama Mwanamuziki wa Circular Music. Alifariki mwaka 2010 jijini Dar es salaam, miaka michache kabla hajafariki Dr Remmy alimpokea YESU kama Bwana na Mwokozi wa MAISHA Yake. Baada ya kuokoka Dr Remmy alikuwa akisali katika kanisa la Glory of Christ  lililoko Ubungo jijini Dar es salaam. Watumishi kanisani hapo walimshauri anyoe Nywele kama moja ya Hatua za Kuvunja maagano yaliyowekwa hapo awali kitendo ambacho Dr Remmy alikubali na kunyoa rasta hizo. 

Baada ya kuokoka Remmy alisema katika maisha yake alikuwa akiudharau wokovu na hakuwahi hata kufikiri kuwa ipo siku atakuja kuokoka au kukata nywele. Biblia inasema  “All things works together for Good”, Safari ndefu ya maisha ya Dr Remmy ikaishia Madhabahuni. Album yake ya Injili aliyoipa jina la “Kwa Yesu kuna Furaha” iligusa mioyo ya watu wengi kwa kuwa ilibeba ushuhuda wa maisha yake.Remmy alibatizwa kanisani hapo kisha akaanza kumtumikia Mungu kama muimbaji wa nyimbo za injili mpaka mwisho wa uhai wake. 

Santos wa Arsenal nje mechi ya Everton

Mlinzi wa kushoto wa Arsenal Andre Santos, ameondolewa katika kikosi kitakachocheza siku ya Jumamosi dhidi ya Everton katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu ya Kandanda ya England baada ya kuumia kifundo cha mguu wakati wa mchezo na Olympiakos.

Andre Santos aumia kifundo cha mguu hatacheza na Everton
Andre Santos
Santos alilazimika kutoka uwanjani dakika ya 51 siku ya Jumanne baada ya Arsenal kulazwa mabao 3-1 katika mchezo wa mwisho wa kundi lao la F kuwania kufuzu kwa hatua ya mtoano ya Ubingwa wa Ulaya.

Hhc Alive ina habari kuwa Santos, ambaye ameshacheza tangu mwanzo mechi 12 za Arsenal katika mashindano yote msimu huu, huenda akakosa mechi hiyo moja tu dhdi ya Everton.

Walinzi wengine wa pembeni wa Arsenal Carl Jenkinson, Kieran Gibbs na Bacary Sagna nao wagonjwa.

Gibbs anaendelea kupata nafuu baada ya kufanyiwa upasuaji wa mshipa wa ngiri mwezi uliopita na hatazamiwi kucheza mechi na Everton, wakati Jenkinson anakabiliwa na maumivu ya mgongo.

Sagna alivunjika mguu wakati Arsenal ilipolazwa na Tottenham mwezi wa Oktoba.

Wenger huenda akalazimika kumchezesha nafasi ya ulinzi wa kushoto Thomas Vermaelen kutokana na walinzi wa kutumainiwa wa pembeni karibu wote kuumia.

Santos, ambaye amshacheza mechi 22 za kimataifa kwa timu yake ya taifa ya Brazil, alijiunga na the Gunners msimu huu akitokea klabu ya Uturuki ya Fenerbahce kwa kitita cha paundi milioni 6.

Rwanda kumenyana na Sudan nusu fainali

Rwanda itacheza dhidi ya Sudan katika nusu fainali ya Kombe la Cecafa Senior challenge kwa nchi za Afrika mashariki na kati. 

Timu zote mbili zilifuzu kufuatia ushindi katika robo fainali siku ya Jumatatu.
Sudan waliwaondoa Burundi kwa kuwafunga mabao 2-0, ilhali Rwanda ilifuzu baada ya kuishinda Zanzibar mabao 2-1.

Amir Abdelnabi aliifungia Sudan katika kipindi cha kwanza, na bao la pili likafungwa na Musa Mohamed katika kipindi cha pili.

Rwanda ilifanikiwa kuibandua Zanzibar kufuatia bao la ushindi lililofungwa na Meddie Kagere dakika mbili kabla ya mechi kumalizika.

Amavubi walikuwa wameshafunga bao la kutangulia katika dakika ya 39 kupitia Jean Baptiste Mugiraneza, lakini muda mfupi baadaye Abdulrahman Mohammed akaisawazishia Zanzibar.

Robo fainali mbili zinachezwa Jumanne, huku Uganda ikichuana na Zimbabwe, nao wenyeji Tanzania bara wakipambana na Malawi.

Washindi kwenye robo fainali hizo ndio watakaokutana katika nusu fainali ya pili.
Nusu fainali kati ya Rwanda na Sudan itachezwa siku ya Alhamisi.

Chelsea yafuzu hatua ya mtoano Ulaya

Andre Villas-Boas amesema Chelsea imewaumbua waliokuwa wakiwabeza baada ya kufuzu hatua ya mtoano ya Ubingwa wa Soka kwa vilabu vya Ulaya kwa ushindi mnono dhidi ya Valencia.
Didier Drogba aifungia Chelsea mabao mawili
Didier Drogba aliifungia Chelsea mabao mawili
Meneja huyo wa Chelsea aliyasema hayo baada ya timu yake kuilaza Valencia mabao 3-0, akiongeza ilikuwa "mateso" kwa klabu yake kwa siku za karibuni kutona na kiwango chao kuporomoka.
"Wachezaji wangu wanastahili heshima ambayo hawapewi," alisema Villas-Boas.
"Tumekuwa tukisumbuliwa na watu mbalimbali tofauti na chagizo zikizidi. Sasa tumewazaba kofi la uso wote hao."

Ushindi huo muhimu wa Chelsea dhidi ya Valencia ulikuwa ni watano katika mechi 11 zilizopita lakini ulitosha kwa timu hiyo kumaliza wakiwa vinara wa kundi E wakifuatiwa na Bayer Leverkusen ya Ujerumani, waliotoka sare na Genk.

Na Villas-Boas alitumia nafasi hiyo kuvishambulia vyombo vya habari kwa namna vilivyokuwa vikitangaza habari za timu yake.

Anahisi vinara wa Ligi Kuu ya England Manchester City hawamo kwenye chagizo kubwa kutoka kwa vyombo vya habari, hata wanapokalia kuti kavu kuelekea kuondolewa hatua ya makundi ya Ubingwa wa Ulaya, walipolazwa na Napoli.

"Natumai Manchester City watafuzu hatua ya mtoano ya Ubingwa wa Ulaya lakini namna vyombo vya habari vilivyokuwa vikiandika kuhusu wao, iwapo watafuzu watakuwa wamefuzu, iwapo hawatafanikiwa kufuzu watakuwa hawajafanikiwa, jambo ambalo vyombo vya habari vilikuwa haviandiki na kutangaza dhidi yetu."
Villas-Boas zaidi hakupendezwa na maoni ya mlinzi wa zamani wa Manchester United na England Gary Neville aliyoyatoa kabla ya mechi yao dhidi ya Valencia.

Nayo Arsenal ililazwa nchini Ugiriki lakini bado imefanikiwa kusonga mbele hatua ya mtoano ya Ubingwa wa Ulaya baada ya kumaliza ikiongoza kundi F.

Mabao yaliyofungwa na Rafik Djebbour, David Fuster na Francois Modesto yaliipatia Olympiakos ushindi wa mabao 3-1- lakini walishindwa kufuzu baada ya Marseille kushinda mchezo wao dhidi ya Dortmund.
Yossi Benayoun aliifungia Arsenal bao hilo moja la kufutia machozi kwa mkwaju wa yadi 15.

Lakini mbali ya kupoteza mchezo huo, usiku ulikuwa mbaya kwa Arsenal baada ya mlinda mlango Lukasz Fabianski na mlinzi wa kushoto Andre Santos walitolewa nje baada ya kuumia.

Haukuwa mchezo mzuri uliooneshwa na Arsenal ambao Wenger angependelea wakati mechi hiyo ya jana alikuwa akitimiza mchezo wa 200 tangu aanze kuisimamia mechi za Ulaya, mechi 44 alipokuwa Monaco na 156 kwa Arsenal.

Tanzania na Uganda nusu fainali

Kombe la Cecafa
Kombe la Cecafa
Uganda itamenyana na wenyeji Tanzania Bara katika nusu fainali ya Kombe la Cecafa siku ya Alhamisi, baada ya timu zote mbili kushinda katika mechi za robo fainali siku ya Jumanne mjini Dar es salaam.

Uganda Cranes waliishinda Zimbabwe 1-0 katika mechi ya kwanza, nao Kilimanjaro Stars wakawafurahisha mashabiki wa nyumbani kwa kuifunga Malawi 1-0 katika robo fainali ya mwisho.
Bao lao la Tanzania Bara la ushindi lilifungwa na Nurdin Bakari katika dakika ya 35, kwa kukamilisha pasi kutoka Mrisho Ngasa.

Tanzania Bara ndio mabingwa watetezi wa kombe hilo.
Zimbabwe waliudhibiti mchezo dhidi ya Uganda lakini wakakosa bahati ya kufunga.
Hamis Kiiza ndiye aliyefungia Uganda bao hilo moja.
Nusu fainali nyingine siku ya Alhamisi itakuwa kati ya Sudan na Rwanda.

Saadi Gaddafi 'ajaribu kupenya Mexico'


Saadi Gaddafi
Serikali ya Mexico imesema imezuia njama iliyokuwa ifanywe na kundi la wahalifu la kumpenyeza kwa magendo mmoja wa watoto wa aliyekuwa kiongozi wa Libya Kanali Muammar Gaddafi nchini Mexico.
Saadi Gaddafi amekuwa kwenye kifungo cha nyumbani nchini Niger iliyopo Afrika Magharibi tangu alipoikimbia Libya mwezi Septemba.
Msemaji wa serikali ya Mexico alisema Saadi Gaddafi na baadhi ya wanafamilia wake walizuiwa kutokana na matokeo ya ripoti za kijasusi.
Watu wengi wamekamatwa kutokana na tukio hilo.
Maafisa wa Mexico wamsema jaribio hilo- lililoibuliwa Septemba 6- lilihusisha majina na nyaraka za uongo.

Waziri wa mambo ya ndani Alejandro Poire alisema mpango huo unahusisha mtandao wa uhalifu " mkubwa wa kimataifa", lakini ikagundulika mwezi Septemba kabla ya mpango huo kukamilika.


Mtandao huo ulihusisha watu kutoka nchi mbalimbali, ikiwemo Mexico, Denmark na Canada, Bw Poire aliuambia mkutano wa waandishi wa habari huko Mexico.
Alisema, walikuwa wakinunua nyumba zenye salama na kufungua akaunti za benki.
Tarehe 14 Septemba- siku nane baada ya njama hiyo kugundulika- Niger ilisema Saadi Gaddafi, mwenye umri wa miaka 38, aliwasili mjini Niamey.
Iliripotiwa kuwa alisafirishwa kwa ndege ya kijeshi kutoka mji wa Agadez kaskazini mwa nchi hiyo.

Septemba 29, Shirika la polisi la kimataifa, Interpol lilitoa " hati ya kukamatwa" kwa Saadi Gaddafi, wakitaka nchi wanachama imkatae iwapo atatokea kwenye nchi zao.
Wakala wa polisi wa kimataifa wamesema anatakiwa kwa madai ya kutoa vitisho kwa kutumia silaha alipokuwa mkuu wa shirikisho la mpira la Libya.

Saadi Gaddafi, ambaye alikuwa akicheza soka katika ligi kuu ya Italia Serie A, pia amewekewa vikwazo vya kusafiri na mali zake kutiwa tanji chini ya azimio la baraza la usalama la umoja wa mataifa lililopitishwa mapema mwaka huu.

Kirk Franklin amaliza ziara yake Barani Africa



Kirk Franklin
Mwanamuziki wa injili kutoka nchini Marekani Kirk Franklin Tarehe 5 DEC 2011 amefanikiwa kufanya Tamasha la Muziki wa injili nchini Zambia. Katika tamasha hilo lililohudhuriwa na umati wa watu, Kirk kabla ya kufanya tamasha nchini zambia alitokea Nchini Nigeria ambako walifanya tamasha siku ya Ijumaa tarehe 2 Dec 2011. Kirk mwenye miaka 41 baada ya Concert la nchini Zambia alielekea Harare nchini Zimbabwe kwa Concert lingine lililofanyika jana Tarehe 6/12/2011.

Wakati alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Keneth Kaunda jijini Lusaka, Kirk aliwaambia waandishi wa habari kuwa “ moja kati ya maazimio ya Ziara hiyo ni pamoja na kuangalia uwezekano kufanaya kazi na wanamuziki wa injili wa nchini humo ili kuwasaidia katika kutimiza ndoto zao.